Posts

WATAKAO KISANUKISHA TAREHE 1/06/2012 NDANI YA ROCK CITY NI JAGUAR ALONG SIDE DJ ZERO

Image

RIPOTI: PICHA ZA TUKIO ZIMA LA MAANDAMANO YA WAZANZIBARI KATIKA HARAKATI ZA KUPINGA MUUNGANO WA TANZANIA

Image
 Mmoja wa waandamani wa Kundi la Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislam (JUMIKI) Kisiwani Unguja,Zanzibar akionyeshan kitambaa kilicho na Damu mapema leo Asubuhi wakati wakiendelea na maandamano yao ambayo yamesababisha vurugu kubwa kisiwani humo,iliyopelekea kuchomwa moto kwa moja ya makanisa pamoja baadhi ya magari yaliyokuwa yameengeshwa karibu na njia wapitazo.vurugu hizo zimeanza jana usiku baada ya kukamatwa kwa kiongozi wa Juimuiya hiyo.  Waandamanaji wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislam (JUMIKI) wakiendelea na maandamano yao mapema leo asubuhi.  Askari wa Jeshi la Polisi kikosi cha kuzuia Ghasia wakifanya doria katika mitaa mbali mbali ya Zanzibar mapeka leo asubuhi. ***************** Baadhi ya wananchi wa Zanzibar kwenye kisiwa cha Unguja, wameandamana kupinga muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar inayopelekea kua Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.  Maandamano hayo yameleta mchafuko unaoendelea Zanzibar, huku i...

FID Q: Nikistaafu Muziki, Ningependa kuwa kama Profes Shivji

Image
Rapper mashuhuri nchini Tanzania, Fareed Kubanda aka Fid Q amesema kama akistaafu kufanya muziki angependa kuwa Profesa kama alivyo Profesa Issa Shivji. Profesa Shivji ni mhadhiri Mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika masuala ya sheria. Fid ambaye anajulikana sana kwa utunzi wa mashairi mazito, alikuwa akijibu swali la shabiki katika utaratibu aliojiwekea kila weekend wa kujibu maswali kupitia Twitter. Kuhusu swali lililomuuliza kama ana mpango wowote wa kujiingiza kwenye siasa kama walivyofanya wasanii wengine husasan Joseph Mbilinyi aka Sugu ambaye ni mbunge wa Mbeya mjini, Fid aka Ngosha amesema bado hana mpango huo kwa kujibu, “bado lakini juzi nilikutana na msafara wa John Mnyika nikavutiwa na zile shamrashamra!” Rapper huyo kutoka Mwanza anayejulikana kwa kuwa msomaji mzuri wa vitabu husasan vya filosofia amemtaja Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kama mwanafilosofia anayempenda zaidi katika muda wote (all time favourite philosopher). source www.freebongo.blo...

Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia,Mh. January Makamba atembelea Airtel Tanzania

Image
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba (kushoto) akipokewa na Mkurugenzi Mtendai wa Airtel Tanzania,Sam Elangallor, alipofanya ziara kukagua shughuli mbalimbali za kampuni hiyo jijini Dar es Salaam leo. Katikati ni Mkurugenzi wa Mawasilino wa Airtel, Beatrice Singano Mallya. Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba (kushoto) akipokewa na Ofisa Mkuu wa Biashara wa Airtel Tanzania, Chiruwi Walingo alipokwenda kufanya ziara ili kukagua shughuli mbalimbali za kampuni hiyo jijini Dar es Salaam leo.Katikati ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel,Beatrice Singano Mallya. Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Tanzania, Beatrice Singano Mallya akiongozana na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba (kushoto) katika ofisi za makamo makuu ya Airtel wakati wa ziara yake kukagua shughuli mbalimbali za kampuni hiyo jijini Dar es Salaam leo. Mkurugen...

MISS NYAMAGANA WAENDELEA KUTESA

Image
Shindano la Miss Nyamagana 2012, Litafanyika katika ukumbi wa Gold Crest Mwanza, tarehe 02/06/2012 ambapo wasanii Linah, Ditto na Hafsa Kazinja watalipamba jukwaa. Mc katika shindano hilo ni msanii maarufu katika tasnia ya uchekeshaji na mzungumzia Mpoki.  Jumla ya warembo 20 watapanda jukwaani kumpata Miss Nyamagana 2012, kabla ya shindano la kumpata mrembo wa Mkoa wa Mwanza. Katika mahojiano yaliyofanyika, warembo wameonekana kuwa na shauku kubwa ya ushindi, wakiaahidi kurudisha taji la Miss Tanzania Mkoani Mwanza. Shndano la Miss Nyamagana 2012 linaandaliwa na Stoppers Entainment ya jijini Mwanza.

AY akamilisha shooting ya video yake Afrika Kusini

Image
Kazi ya kushoot video ya Ambwene Yesaya aka AY iliyofanyika jijini Johannesburg, Afrika Kusini imemalizika salama jana. AY aliambatana na producer wa wimbo huo uliokuwa ukifanyiwa video, Marco Chali wa Mj Records. Video hiyo ambayo kwa mujibu wa AY imegharimu $20,000 ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 30 za Tanzania, imeongozwa na director wa Nigeria anayeishi nchini Afrika Kusini Mike Ogeke wa kampuni ya GodFather Productions. Wakati wa shooting hiyo wanamuziki mapacha wa kundi la P-Square, Peter na Paul Okoye walikuwepo japo haijulikani kama wataonekana kwenye video ya AY kwakuwa nao walikuwa wakifanya video yao na kampuni hiyo. Baada ya kukamilisha shughuli hiyo AY alitweet,” I_Am_Godfather are very professional,great team EVER,we gonna shoot more videos with them.” “Had a great shoot with Tanzanian hottest artist, @AyTanzania! #its a wrap! Good working with you sir!” aliandika mmoja wa watu waliohusika kushoot video hiyo. Katika hatua nyingine AY ames...

Hussein Machozi afanya ngoma na mwanadada Size 8 wa Kenya

Image
Mwanamuziki wa Tanzania Hussein Machozi amefanya ngoma na msanii wa kike Size 8 anayetemba sana kwa sasa nchini Kenya pamoja na Afrika Mashariki. Wimbo huo ambao umefanyika katika studio za Ogopa Djs za nchini humo unaitwa Addicted. Machozi anasema wimbo huo ni kwaajili ya mashabiki wake wa kike ambapo video ya wimbo huo itafanywa na kampuni ya Ogopa DJs. Kwa sasa Size 8 ambaye jina lake halisi ni Linet Masiro Munyali anakimbiza na club banger yake iitwayo Vidonge. Mwaka jana msanii huyo alitajwa kuwania tuzo za Chagua La Teeniez za Kenya kwenye kipengele cha mwanamuziki bora wa kike. Hii si mara ya kwanza kwa Hussein Machozi kumshirikisha msanii wa Kenya kwani tayari ana wimbo alioufanya na mwanadada Habida uitwao Asante.

WAUGUZI WA HOSPITALI YA MKOA WA MARA WAGOMA

Augustine Mgendi Wauguzi katika hospitali ya Mkoa wa Mara wameweka mgomo wa kuingia wodini na kutoa huduma mbalimbali katika hospitali hiyo wakishinikiza uongozi wa hospitali hiyo kuwalipa madai yao mbalimbali ambayo wanadai na kusema kuwa hawatafanya kazi mpaka hapo watakapo tekelezewa. Mgomo huo wa wauguzi umeanza leo asubuhi baada ya wauguzi hao kufika kazini na kushindwa kufanya kazi huku wakisema kuwa wamenyanyaswa vya kutosha na wanachotaka nikulipwa madai yao ndipo huduma kutoka kwao ziweze kuendelea katika hospitali hiyo. Kutokana na mgomo huo kumesababisha usumbufu mkubwa kwa wagonjwa wa wodini na wale wa nje baada ya kukosa huduma mbalimbali huku wengine wakitupia lawama kwa uongozi wa hospitali hiyo kwa kushindwa kukaa na wauguzi hao na kufika muafaka ili waendelelee kupata huduma kama kawaida. Mmoja wa wauguzi wa hospitali hiyo Antunia Machibula alisema kuwa kutokana na kushindwa kuthaminiwa kutokana na kupuuzwa kwa malipo yao na shughuli wanazozifanya wameamua ...

HUKUMU YA JOHN MNYIKA LEO...

Image
Mbunge wa Jimbo la Ubungo,John Mnyika. NI KATIKA HUKUMU YA KESI KUPINGA MATOKEO YA UBUNGE WA JOHN MNYIKA James Magai MAHAKAMA Kuu, Kanda ya Dar es Salaam, leo itawaliza au kuwafurahisha wapenzi na wanachama wa Chadema wakati itakapotoa hukumu ya kesi ya kupinga matokeo ya ubunge yaliyompa ushindi Mbunge wa Jimbo la Ubungo kupitia chama hicho, John Mnyika. Kesi hiyo namba 107 ya 2010, ilifunguliwa na aliyekuwa mgombea wa CCM, Hawa Ngh’umbi dhidi ya Mnyika ambaye ni mdaiwa wa pili katika kesi hiyo akitetewa na Wakili Edson Mbogoro. Mdaiwa wa kwanza katika kesi hiyo iliyoko mbele ya Jaji Upendo Msuya ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na aliyekuwa Msimamizi wa Uchaguzi (RO) katika jimbo hilo, (aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni) ambao walikuwa wakitetewa na Wakili Mkuu wa Serikali (PSA), Justice Mulokozi. Katika uchaguzi huo, uliofanyika Oktoba 31, 2010, Msimamizi wa Uchaguzi, Raphael Ndunguru alimtangaza Mnyika kuwa mshindi Novemba 2, 2010 baada ya kupata kura 66,742. Ngh...

KANYE WEST NA BEYONCE WAONGOZA KATIKA KUWANIA TUZO ZA BET 2012

Image
Majina ya wanaowania tuzo za BET kwa mwaka 2012 yamewekwa wazi. Wanaoongoza kwa kuteuliwa kuwania tuzo nyingi ni Beyonce aka Mrs Jigga na shemejie Kanye West.Wakati Beyonce anawania tuzo 6,Kanye anawania 7. Washindi wa tuzo za BET mwaka huu watatangazwa katika show maalumu itakayofanyika tarehe 1 Julai kutokea Shrine Audotorium huko Los Angeles. Mwigizaji maarufu, Samuel L.Jackson ndiye atahost show ya mwaka huu. Hii hapa chini ni orodha kamili ya walioteuliwa kuwania tuzo hizo na vipengele vyake Best Female R&B Artist Marsha Ambrosius Beyoncé Mary J. Blige Melanie Fiona Rihanna Best Male R&B Artist Chris Brown Bruno Mars Miguel Trey Songz Usher Best Male Hip-Hop Artist Big Sean Drake J. Cole Lil Wayne Rick Ross Young Jeezy Best Female Hip-Hop Artist Nicki Minaj Diamond Trina Brianna Perry

VIMWANA MISS NYAMAGANA HAWA HAPA!!!

Image
Shindano la Miss Nyamagana 2012, Litafanyika katika ukumbi wa Gold Crest Mwanza, tarehe 02/06/2012 ambapo wasanii Linah, Ditto na Hafsa Kazinja watalipamba jukwaa. Mc katika shindano hilo ni msanii maarufu katika tasnia ya uchekeshaji na mzungumzia Mpoki. Jumla ya warembo 20 watapanda jukwaani kumpata Miss Nyamagana 2012, kabla ya shindano la kumpata mrembo wa Mkoa wa Mwanza. Katika mahojiano yaliyofanyika, warembo wameonekana kuwa na shauku kubwa ya ushindi, wakiaahidi kurudisha taji la Miss Tanzania Mkoani Mwanza. Shndano la Miss Nyamagana 2012 linaandaliwa na Stoppers Entainment ya jijini Mwanza. Vimwana wakipata flash.. Vimwana wa Nyamagana na flash...   SOURCE www.gsengo.blogspot.com  

Redds Miss Chan'gombe hiyooo yaja!!

Image
  Wanyange wanaowania taji la Redds Miss Cha'gombe 2012 wakiwa katika picha ya pamoja iliyopigwa muda mfupi baada ya kumaliza mazoezi yao jana katika ukumbi wa TCC Chan'gombe jijini Dar es Salaam. Warembo hao 11 wanataraji kupanda jukwaani mapema mwezi ujao kuwania taji hilo na kuwania tiketi ya kushiriki Miss Temeke 2012.

MADEREVA WA BODABODA MJINI MUSOMA WAPEWA SOMO

Na Shomari Binda Musoma, Madereva wa pikipiki zinazobeba abiria maarufu kama bodaboda mjini Musoma wametakiwa kuwa makini na kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuweza kuepuka ajali ambazo zinaweza kusababisha vifo na majeruhi kwa abiia na waendeshaji wa pikipiki na hivyo kusababisha kupunguza nguvu kazi ya Taifa. ... Kauli hiyo imetolewa na muuzaji na msambazaji wa pikipiki aina ya Toyo Mjini hapa Seif Pazi alipokuwa akizungumza na madereva wa pikipiki katika viwanja vya Shule ya msingi Mukendo katika kuwakumbusha umuhimu wa kuzingatia sheria wawapo barabarani na kusema katika ufatiliaji uliofanywa na wadau mbalimbali wa usalama barabarani umebaini ajali nyingi nyingi za pikipiki zinatokana na kutokuzingatia sheria. Alisema ajali nyingi zinaweza kuepukika iwapo madereva watakuwa makini pindi waendeshapo vyombo vyao na kuvifanyia uchunguzi wa mara kwa mara ili kuweza kuvifanyia matengenezo kwa vile vinavyohitaji matengenezo kwani kwa kufanya hivyo kutapel...

Waziri Akumbana Na Madudu Maliasili

Image
 WAZIRI mpya wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, ameelezea kushtushwa kwake na ubadhilifu wa kutisha ulioko katika wizara hiyo, Idara ya Wanyamapori unaodaiwa kufanywa na baadhi ya watendaji wake.   Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuzindua Bodi ya Ushauri ya Wizara ya Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) jijini Dar es Salaam, jana, waziri huyo alisema idara hiyo inanuka kwa uozo unaotokana na wizi na ubadhilifu mkubwa ambao umeleta hasara kwa taifa.   Kagasheki alidai idara hiyo inaongoza kwa madudu ya kutisha, na ametangaza kuchukua hatua za haraka dhidi ya watendaji wanaotuhumiwa kuhusika na ubadhilifu huo mkubwa haraka iwezekanavyo, akidai fedha zilizotafunwa na wajanja hao ni nyingi.   “Jamani Idara ya Wanyamapori ina fedha nyingi, lakini zinaliwa na watu kwa maslahi binafsi, na kama fedha hizo zingekuwa zinapelekwa serikalini kama inavyohitajika, nchi hii kwa sasa in...

Ajari Mbaya Yatokea Iringa

Image
Askari wa usalama barabarani mjini Iringa wakiwa wamebeba moja kati ya maiti za ajali ya Taxi na Fuso iliyotokea eneo la kituo cha Mafuta Eso kwenye barabara kuu ya Iringa -Mbeya asubuhi hii Wananchi wakitazama Fuso ambalo liligongana na Taxi hiyo Miili ya wafanyakazi wa barabara Iringa ambao walikufa katika ajali hiyo Wananchi na polisi wakisaidiana kuinasua miili ya watu watatu walio kufa katika ajali Hivi ndivyo Fuso hilo lilivyokuwa baada ya ajali Mwili wa dereva Taxi ukiwa bado kutolewaAjali mbaya imetokea mjini Iringa asubuhi hii na kusababisha vifo vya watu watatu papo hapo huku abiria waliokuwemo katika fuso wakinusurika katika ajali hiyo .   source www.freebongo.blogspot.com

picha: Annular Eclipse, May 2012

Image
 Ni nadra kuona "annular eclipse" ambapo mduara unaotokana na miale ya mwanga wa jua la machweo huonekana kuuzunguka mwezi ambao kwa wakati huo ndiyo unakuwa ukichomoza na kupita kati ya jua na sayari ya Dunia. Tofauti na kupatwa kabisa kwa jua (total solar eclipse), kwenye 'annular eclipse' mwezi huwa na umbo dogo linaloshindwa kulifunika jua lote, hivyo ile sehemu ya jua inayobaki bila kuzibwa, mwanga wake ndiyo unaoonekana kuuzunguka mwezi na kutengeneza mduara wenye mfano na umbo la pete. Juzi ilitokea "annular eclipse" na baadhi ya vyombo vya habari viliwakumbusha watu kubeba zana zao za kukinga macho na kisha kushuhudia hali hyo ambayo ni nadra sana kutokea. Jumapili, annular eclipse ilishuhudiwa magharibi mwa Texas, Arizona, Oregon bahari ya Pasifiki hadi Tokyo, Japan. Picha hizi na nyingine zaidi zipo katika tovuti ya  boston.com/bigpicture                       ...

"The Spear" depicting Jacob Zuma with genitalia in the open has been vandalized

Image
                         image: zapiro.com A painting supposedly of South Africa’s President Jacob Zuma showing his genitals and the subject of a court challenge by the ruling African National Congress party has been defaced at a Johannesburg gallery. Two men smeared paint on the portrait, known as “The Spear,” which depicts Zuma in black, yellow and red in a pose similar to one in which former Russian leader Vladimir Lenin was frequently shown in Soviet propaganda posters, footage broadcast on eNews Channel showed today. The South Gauteng High Court was to hear an application to have it removed after the ANC said it infringes on Zuma’s constitutional right to dignity and privacy. The party will continue with its application on principle as the president had been humiliated, spokesman Jackson Mthembu said in an interview. ANC supporters gath...

Rais Kikwete ateua majaji wa Mahakama ya RUfani

T AARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amewateua Majaji wawili wa Mahakama Kuu ya Tanzania kuwa Majaji wa Mahakama ya Rufani. Walioteuliwa ni Jaji Semistodes S. Kaijage na Jaji Kipenka M. Musa na kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo, Jumatatu, Mei 21, 2012 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Y. Sefue, uteuzi wao ulianza tokea Machi 15, mwaka huu, 2012. Kabla ya kuteuliwa kwake kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jaji Kaijage (57) alikuwa Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam tangu Mei 17, 2007. Aliteuliwa kuwa Jaji Mahakama Kuu Novemba 28, mwaka 2000. Naye Jaji Musa (57) alikuwa Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu Kanda ya Tanga kabla ya kuteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani. Pia amewahi kuwa Wakili wa Serikali, Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba. Aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu Septemba 13, 2004. Imetolewa na: Kuru...

Picha za Tamasha la UTAMADUNI WETU v/s BONGO FLAVA

Image
Mkuu wa Wilaya ya Moshi Dkt. Ibrahim Msengi amezindua tamasha la Utamaduni Wetu v/s Bongo Flava lililofanyika katika viwanja vya Mandela vilivyopo katika kata ya Pasua, katika Manispaa ya Moshi ambalo limehusisha nyimbo mbalimbali ikiwemo za asili, zinazouenzi utamaduni wa makabila mbalimbali. Dkt. Msengi amesema moja ya mambo ambayo yanaendelea kuubomoa kama siyo kutokomeza kabisa  utamaduni wa Watanzania ni pamoja na utandawazi ambao umekuwa ukichangia wananchi hususani vijana kushabikia tamaduni za Magharibi   na kusahau tamaduni za Kiafrika. Mkuu huyo wa Wilaya amesisitiza kuwepo  umuhimu wa waannchi kuendelea kuuenzi utamaduni wao. Akasema, mahali popote utakapokwenda, vitu kama vile lugha, mavazi au chochote kinachokubalika kuutambulisha utamaduni, huwa ndicho kitambulisho husika cha mtu na utamaduni wake. Naye mratibu wa tamasha hilo, Ismail Mnikite wa Endeleza Foundation amesema lengo la tamasha hilo ni kuhamasisha, kuendeleza na kuimaris...

PICHA ZA LINAH AKIWA MAREKANI.

Image
  Mwimbaji LINAH SANGA ambae yuko Marekani kupiga show kwa muda wa miezi minne, hapo yuko na 2012 Chevy Camaro Convertible in California, jana alipiga show Cafe Randevous at 2430 Broadway St.  Oaklan. ..