Tuesday, May 29, 2012

CHADEMA YAITEKA MTWARA

chadema mtwara  
Aliekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Mh Godbless Lema akihutubia maelfu ya wananchi wa Mtwara katika Viwanja vya Mashujaa jana. CHADEMA wako mikoa ya kusini mwa Tanzania kwa ziara ya kuimarisha chama hicho katika maeneo hayo na pia kuutanzaza mapango wao mpya wa kuwashirikisha wananchi katika shuguli za chama (Movement for Change-M4C) kuanzia jana hadi Juni 11, 2012
*********
DHANA ya kuwa mikoa ya kusini ni ngome ya Chama cha Mapinduzi jana ilifutika vichwani mwa wakazi wa mikoa hiyo, baada ya umati mkubwa kujitokeza, kuulaki msafara wa viongozi na hatimaye kuhudhuria mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Mashujaa, mkoani Mtwara. 

Msafara huo wa kitaifa ukiongozwa na Mwenyekiti Freeman Mbowe, ulipata mapokezi ya vijana wakiwa katika msafara wa pikipiki magari na baiskeli karibu na daraja la Mikindani na kuelekea katika uwanja wa Mashujaa ambapo umati mkubwa wa watu ulifurika kupita kiasi. 

Akihutubia katika mkutano huo Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Freeman Mbowe alisema ameshajiandaa kisaikolojia kufa kwa ajili ya kutetea haki na kwamba wananchi wasiogope kupigania haki zao. 

Alisema ikitokea akafa akiwa katikati ya mapambano waliobaki wasihuzunike bali wahakikishe huo ndiyo unakuwa mwanzo wa ukombozi. 

“Nikifa katika mapambano haya uinueni mwili wangu uwekeni pembeni na kisha endeleeni na mapambano kwa kuwa haya si ya Mbowe peke yake bali ni ya Watanzania wote,” alisema Mbowe.
Aliwaambia wakazi wa Mtwara kuwa hawakwenda pale kutafuta jimbo au kata bali kuleta ukombozi wa kweli kwa kuwa ni wajibu wa kila Mtanzania kuhakikisha nchi inakombolewa. 

Akizungumzia kuhusu udini, Mbowe alisema viongozi wa serikali wanaotumia udini, ukabila na ukanda kuwagawa watu wamekata tamaa ya kuwatumikia. 

Alisema kuwa kwa hali ilivyo itakuwa ni hatari zaidi kwa ustawi wa Tanzania kama hata tone moja la mafuta yatapatikana huku nchi ikiwa inaongozwa na serikali ya CCM kwa kile alichodai tayari wamemwaga damu kwa tamaa ya mali katika rasilimali zilizokwishaanza kupatikana. 

Naye Katibu mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa, aliwataka polisi kuacha kuwanyanyasa raia na kueleza hata yanayotokea Zanzibar kwa sasa ni udhaifu wa Rais Jakaya Kikwete wa kutaka kuzuia watu wasitoe maoni. 

Alisema hatua ya kuwataka watu wasijadili suala la Muungano wakati unawagusa haiwezi kukubalika na kwamba polisi wawe na akili ya kuambiwa na kisha kuchanganya na zao kwa ajili ya maslahi ya Tanzania. 

“Kikwete amesababisha hali hii ya Zanzibar, maana hakukuwa na haja ya kumkamata mtu aliyekuwa anatoa maoni juu ya mustakabali wa nchi yake,” alisema Dk. Slaa. 

Kuhusu bajeti ya 2012/2013 Dk. Slaa alitaka isimamishwe na mishahara ya wafanyakazi iboreshwe. 

Kuhusu korosho, Dk. Slaa alisema wakazi wa Mtwara wanafanywa maskini huku korosho zao zikienda kutoa ajira kwa wananchi wa India na wajanja wachache wa hapa nchini. 

“Tanzania haitakombolewa bila mikoa ya kusini kuwa huru, tunataka mtuunge mkono katika kila hatua ili tuchukue nchi 2015,” alisema Dk. Slaa. 

Mnyika adai Bunge ni Kanyaboya
Mbunge wa Ubungo John Mnyika akihutubia umati huo alisema Bunge la Tanzania halina nguvu ya kuiwajibisha serikali na kama litafanya hivyo Rais anaweza kuwatimua wabunge wote. 

Alisema hali hiyo inachangiwa kwa kiasi kikubwa na Katiba liyopo ambayo alisema ni lazima Watanzania wajitokeze na kuingiza mambo ya msingi wakati wa kutoa maoni. 

Aliongeza wakazi wa Mtwara wanashindwa kufaidika na gesi iliyoko mkoani humo pamoja na kukosa uwezo wa kumiliki ardhi kwa amendeleo yao. 

Mawazo abeba silaha
Aliyekuwa diwani wa CCM kata ya Arusha Alphonce Mawazo aliwaambia wakazi wa Mtwara kuwa mabadiliko ya kweli huanza kwenye akili na mtu akishafungua akili kila kitu chake kitaenda kwa ufasaha na kuwa huru. 

Huku akishangiliwa na umati wa watu uwanjani hapo Mawazo alisema wameenda Mtwara wakiwa na silaha za nguvu ya umma, na kuwataka wasitengane katika kutafuta mabadiliko ya kweli, na kuachana na waliowasaliti kwa kuwaingiza katika maisha magumu.
Aliwaeleza wakazi wa Mtwara kuwa wamefungwa na minyororo ya umaskini na kwamba minyororo hiyo ni mibaya kwa mustakabali wa maisha yao kuliko hata minyororo ya chuma waliyokuwa wakifungwa watumwa enzi za ukoloni 

Millya: CCM imeshaanza  kuaga
Kwa Upande wake aliyekuwa Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Arusha James Millya alisema harakati zilizoanzishwa na CCM hivi karibuni kutaka nafasi ya mgombea urais ihojiwe  mahakamani ni baada ya kugundua mwaka 2015 hawatakuwa na nafasi ya kushinda hivyo kimbilio lao ni mahakamani. 

“CCM wanatuaga na mkitaka kuamini hilo sasa wameanza kutaka nafasi ya urais ihojiwe mahakamni kwa kuwa huko ndiko kimbilio lao lililobaki kwa sasa,” alisema Millya. 

Alisema CCM inaichukia CHADEMA kwa kuwa inataka uhakika wa maisha hata kwa mtoto wa maskini ambaye hajui hatma yake ya maisha kwa siku zijazo. 

Aliongeza kuwa ni wakati muafaka sasa kwa Watanzania kuachana na watu waliowasaliti kwa kushindwa kusimamia wajibu waliokabidhiwa. 

Habari na Tanzania Daima, Mei 29. 2012

BASATA YAWATAKA WASANII KUONGEZA THAMANI KATIKA KAZI ZAO

Mtendaji Mkuu wa asasi ya Musoma Handcrafts Haroun Sabili akitoa elimu kwa Wasanii na Wajasiriamali wa Sanaa za mikono kwenye programu ya Jukwaa la Sanaa wiki hii.
Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti, Mafunzo na Habari wa BASATA Godfrey Lebejo akisisitiza jambo wakati akihitimisha programu ya Jukwaa la Sanaa wiki hii. Aliwataka wasanii kuongeza thamani katika kazi wanazozalisha.
Akina mama Wasanii wa Sanaa za mikono wakiangalia moja ya kazi iliyobuniwa na kuongezewa uthamani. Kazi hiyo ilikuwa imetengenezwa na malighafi kutoka masalia ya viumbe wa baharini.
Sehemu ya Wasanii na Wadau wa Sanaa za Mikono waliohudhuria kwenye programu ya Jukwaa la Sanaa wiki wakifuatilia darasa kwa makini.

Na Mwandishi Wetu

Huku kukiwa na juhudi za kutambuliwa na kuthaminiwa kazi za wasanii ndani na nje ya nchi, Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limewataka wasanii kuongeza thamani kwenye kazi zao ili kuzipa ubora zaidi.

Wito huo umetolewa mapema wiki hii na Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti, Mafunzo na Habari wa BASATA Godfrey Lebejo wakati akihitimisha programu maalum iliyohusu Ubunifu, Utengenezaji na Uongezaji thamani katika Kazi za Sanaa kupitia Jukwaa la Sanaa.

Alisema kuwa, ubora katika Sanaa unapatikana pia kwa Wasanii kuangalia wenzao wanafanya nini na wao kupata ubunifu mpya kwa kuongeza vionjo, uthamani na ubunifu binafsi katika kuifanya kazi ya Sanaa kwanza kupendwa na baadaye kupewa thamani kubwa sokoni.

“Ni wazi Wasanii wetu wanapaswa kuzingatia uongezaji uthamani kwenye kazi wanazozifanya. Kubuni kazi ni suala moja lakini kuongeza uthamani katika kazi yako ili ivutie wengi na kuuzika kwa thamani kubwa ni suala lingine la kuzingatia” alisistiza Lebejo.

MTATIRO: HILI LA ZANZIBAR HALIUNGWI MKONO “LABDA NA MWENDA WAZIMU TU”


JULIUS MTATIRO katibu mkuu wa chama CUF Tanzania bara
*********************
Habari za uchomaji wa makanisa Zanzibar katika vurugu za hivi karibuni haziungwi mkono kwa namna yoyote ile. Yeyote anayefanya vitendo hivi ni gaidi kwa sababu anafanya vitendo vya kigaidi. Serikali ya zanzibar ichukue hatua kali sana za kisheria kwa yeyote aliyehusika na vitendo hivi bila kujali yeye ni nani.

Kuchoma makanisa ni jambo la hatari sana, sielewi anayefanya hivi yeye ni dini gani, sijui ni dini ipi inayoruhusu uchomaji wa nyumba za ibada za dini nyingine, ni dini ya shetani peke yake inaweza kufanya hivyo.

Kuna watu wanasema ati ni “waislamu” ndiyo wanafanya vitendo hivyo, mie nakataa, nasema wanaofanya hivyo siyo waislamu.

 Waislamu walioko Zanzibar naowajua mimi ni wakarimu, ni watulivu na wasikivu na wanapenda amani. Hata mapambano ya wafuasi wa CUF na CCM yaliisha kwa wao wenyewe kuridhiana.
Wazanzibari siyo wakatili kiasi hiki. Kuchoma makanisa hakuwezi kufananishwa na kuchoma Mahakama, ikulu,polisi n.k. Uchomaji wa makanisa au misikiti ni uchonganishi mkubwa unaoibua vita mahali pengi duniani. Anayefanya hivyo ana malengo mabaya sana siyo kwa wananchi wa Zanzibar tu bali kwa wananchi wa wa Tanzania kwa ujumla.

Hii ni kwa sababu makanisa yakishachomwa tetesi zinasema wamechoma waislamu(jambo ambalo siliamini), tetesi hizi zikizidi na pakatokea athari kubwa kwa makanisa na labda watu(wakristo) wakachomwa na kufariki ndani ya makanisa hayo, ina maana wakristo watapoteza ndugu zao.

Kama Zanzibar pana wakristo wachache ambao hawawezi kulipiza kisasi cha adui wasiyemjua, lazima ndugu zao wakristo walioko bara watataka kulipiza kisasi kwa wazanzibari(waislamu) walioko Tanganyika ambao wamejenga na kuoa na kufanya biashara Bara na ambao hata ZAN ID(Vitambulisho vya ukaazi vya Zanzibar hawana) – kwamba kwa sheria za uraia za Zanzibar hata wakirudi kesho hawatambuliki kama wazanzibari.

Nakadiria kuwa kuna wazanzibari takribani laki tatu au laki nne walioko Tanganyika. Wengi wao wana maduka na biashara nyingi, wamenunua mashamba yao huku Tanganyika na kwa kweli maisha yao na vifo vyao na maziko yao viko huku Tanganyika kila inapotokea.

HIVI NDIVYO GRADUATION YA SSPRA ILIVYOFANA

Wiki iliyopita siku ya Jumamosi ilifanyika sherehe ya kuwaaga mwaka wa 3 ambao walikuwa ni wanachama wa SSPRA ambapo sherehe hii ya mahafari ilifanyika katika ufukwe wa ziwa Victoria- -Royal Sunset Beach.

Mgeni rasmi katika mahafari hayo alikuwa ni Afsa uhusiano (Public Relations Manager) wa halmashauri ya jiji la mwanza  BW. Joseph Alex Mlinzi. Wanachama 45 walitunukiwa vyeti vyao na wengine 21 kutunukiwa vyeti vya shukrani kwa kuweza kuiongoza vizuri Association mpaka hapa ilipofikia.

Mgeni rasmi .Joseph Mlinzi aliweza kuwapa nasaa wahitimu wote na kuweza kuipongeza  Association kwa kuweza kupiga hatua kubwa sana ukilinganisha na umri wa Association  tangu imeanzishwa...Mgeni rasmi pia aliweza kutoa kiwango cha shilingi Million 1 na laki 2(1,200,000) kwa ajili ya kuweza kuimarisha mfuko wa chama.
Zifuatazo ni baadhi ya picha ambazo zilichukuliwa wakati wa sherehe hiyo.
Mgeni Rasmi Joseph Mlinzi ambaye ni Meneja Uhusiano wa jiji la Mwanza akiingia ukumbini.
Mwenyekiti wa SSPRA akisoma risala

Keki ikibarikiwa na mgeni rasmi.
Viongozi wa SSPRA wakiwa meza kuu

ILIPENDEZAJE
KUTOKA KUSHOTO NI MC, JACQUELINE PATRICK,  CHEBI,NGONYANI NA ATHANASI

Wageni waalikwa wakiwa meza kuu pamoja na mgeni rasmi.
Makamu Mwenyekiti Bw.Chebi akitoa maelezo mbalimbali kwa wageni

Vijana wa Kigomaaa wakitoa show yao ambayo ilivutia wageni na waagwa

Mwl.Denis Mpagaze pia alikuwepo
Wanachama wa mwaka wa Tatu wakitoa burudani kwa mgeni Rasmi

Mwl.Albert Tibaijuka akimpongeza mwenyekiti wa kwanza wa SSPRA Bw.Yusuf Manning




Wanachama wa mwaka wa pili wakitoa show yao

Njumai and Glory
Creator Francis akipata Msosi
Nyanja kutoka kushoto,Mwambeja,Mudy
                                
Tulitokelezeaje?single button kama kawa.
                                















Monday, May 28, 2012

DIAMOND NA JOKATE WAMWAGANA



PENZI motomoto kati ya mwanamuziki wa Bongo Fleva, Naseeb Abdul ‘Diamond’ na Mrembo Nambari 3 wa Tanzania 2006, Jokate Mwegelo limedaiwa kuvunjika

Kwa mujibu wa chanzo chetu, raia wa Tanzania anayecheza mpira wa kikapu nchini Marekani, Hasheem Thabit Manka anatajwa kuwa chanzo cha penzi la wawili hao kusambaratika.


Awali, Thabit aliwahi kuripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari kwamba ‘anatoka’ na Jokate, madai ambayo kwa upande wake mrembo huyo aliyakanusha vikali akisema anasingizwa licha ya kujikanyaga katika maelezo yake.

Hata hivyo, baadaye wawili hao ikasemekana wamemwagana kwa sababu ambazo hazikuwa wazi kwa vile uhusiano wao ulikuwa wa siri kubwa.
Safari hii, kwa mujibu wa chanzo chetu, Hasheem amemrudia Jokate kwa nguvu zote huku ikidaiwa kwamba hitimisho la uhusiano wao litaishia kwenye kufunga ndoa na kuishi kama mke na mume.


Sosi mmoja alimjulisha paparazi wetu kwa staili ya kumuuliza swali kama anafahamu lolote kuhusu wapenzi hao kupeana mkono wa kwaheri.

“Hivi jamani mnajua kama Jokate na Diamond wamemwagana? Demu amerudiana na Hasheem Thabit, tena safari hii watafunga ndoa kabisa,” alisema sosi huyo.

Akazidi kudai kuwa mbaya zaidi, Jokate amekata waya wa mawasiliano kati yake na Diamond, hali ambayo inampa wakati mgumu jamaa kwani uhusiano wao umevunjika huku akiwa bado anampenda.


Ili kupata uhakika wa madai haya, paparazi wa Risasi alimsaka Diamond kwa njia ya simu ambapo alipopatikana na kuulizwa kuhusu madai hayo, alikuwa na haya ya kusema:

“Hamna, hamna kitu kama hicho. Unajua mambo kama hayo msiandike. Mimi nitaondoka keshokutwa kwenda kufanya shoo Big Brother, si umesikia?”

Paparazi: Yeah! Tumesikia, habari tayari ipo kwenye gazeti.
Diamond: Basi ndiyo hivyo, hiyo habari ya Jokate bwana hamna kabisa.

Baada ya kuongea na Diamond, paparazi wetu alimtwangia simu Jokate ambapo alisikiliza madai mwanzo hadi mwisho lakini badala ya kujitetea au kufafanua, alikata simu.

WEMA ATOA LA MOYONI
Kwa upande wake, aliyekuwa mchumba wa Diamond, Wema Sepetu alipoulizwa kuhusu kuvunjika kwa uhusiano wa wawili hao, alisema:

“Nilisema mimi mkanipuuza, sasa mmekiona alichokifanya Jokate? Naamini ni laana yangu kwani mimi sikuwahi kumfanyia jambo lolote baya Diamond. Mungu ameona, amenilipia. Teh! Teh! Teh!

HIVI NDIVYO DIAMOND ALIVYOPERFORM KATIKA EVICTION PARTY YA BIG BROTHER (BBA 7)

Diamond alikuwa nchini Afrika Kusini Jumapili hii kwa ajili ya performance maalum wakati wa Eviction Party ya Big Brother Africa.Hivi ndivyo ilivyokuwa performance yake BBA7

Dkt. Bilal azindua vitabu vya Yussuf R. Makamba: Binadamu na Kazi; Ukweli kwa mujibu wa Biblia, Kurani Tukufu, Suna za Mtume (SAW) na Sheria za Nchi

Picture

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Makamu wa Rais, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akionesha Kitabu cha Binadamu na Kazi baada ya kukizindua kitabu hicho kilichotungwa  na Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM, Yussuf Makamba (kulia) wakati ya uzinduzi uliofanyika tarehe 27 Mei 2012 kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mke wa katibu huyo, Mama January Makamba. 
Picture

HOTUBA YA NAIBU KATIBU MKUU CHADEMA,MH.ZITTO KABWE KWA WANA-CHADEMA NA WATANZANIA NCHINI MAREKANI

Tumekutana leo wakati ambao Taifa letu lipo katika mpito wa mambo mengi sana.

Kufuatia shinikizo kubwa kutoka chama chetu cha CHADEMA na asasi nyingine za kiraia ikiwemo viongozi wa dini, tupo katika mchakato wa kuandika upya katiba ya nchi yetu. Lakini pia kuna muamko mkubwa sana wa haki za kiraia na haki za kisiasa katika Taifa letu hivi sasa. Watanzania, kuliko wakati mwingine wowote katika historia ya nchi yetu, wameamka na kutaka mabadiliko ya kisiasa na hasa kutaka kabisa uongozi mpya wa nchi kutoka chama kingine tofauti na chama kinachoongoza hivi sasa. Huu mpito pia, Mpito wa kutoka chama kimoja hodhi kwenda mfumo wa kweli wa vyama vingi vya siasa. Watanzania wameamka sana kujua rasilimali za nchi yao na kutaka kutokomeza rushwa na ufisadi na matumizi mabaya ya utajiri wa nchi. Huu ni mpito wa kutoka viongozi wanaojali maslahi yao binafsi na kwenda kwa viongozi wawajibikaji na wenye uchungu wa kuendeleza nchi yetu na watu wake.

Mpito wowote unapaswa kuongozwa vyema. Unapaswa kushirikisha wananchi wote bila kujali wapo sehemu gani ya Dunia. Chama chetu kipo mstari wa mbele kuongoza mpito tulionao Tanzania. Licha ya kuongoza juhudi za kuwa na Katiba mpya itakayohakikisha HAKI na Wajibu wa Watanzania, lakini pia tumekuwa tukiendelea kupambana na rushwa na ufisadi. Pia tumekuwa tukiendelea kuhakikisha utajiri wa nchi  yetu unatumika kwa manufaa ya Watanzania. Hatujatetereka hata kidogo na hatutateterekea kuhakikisha Watanzania wanakuwa na Taifa lenye demokrasia iliyokomaa, lenye maendeleo na ustawi wa watu wake (Developmental Democratic State).

Licha ya kwamba tupo Upinzani, lakini hatua mbalimbali tulizochukua zimeleta mabadiliko makubwa katika nchi yetu. Kuanzia vuguvugu la Buzwagi mpaka kuibuliwa kwa maskandali ya EPA na mpaka kutajwa kwa orodha ya Mafisadi nchini pale MwembeYanga. Hata hivi karibuni juhudi za Bunge kutaka Uwajibikaji Serikalini zilizoongozwa na CHADEMA zimeleta mabadiliko. Inawezekana mabadiliko hayo sio kama tutakavyo, sio kamili, lakini ni hatua ambayo tumepiga. Tutaendelea kama chama cha siasa sio tu kusema na kupiga kelele kuhusu uoza uanaofanyika Serikalini (maana ndio kazi yetu kikanuni) lakini pia kutoa masuluhisho ya matatizo ya nchi yetu na kusukuma kupitia Bunge mabadiliko chanya yanayotakiwa ili kuleta mabadiliko nchini.

BIFU JIPYA CYRILL NA OMMY LAIBUKA....


BAADA ya msanii aliyevuma na wimbo Nai Nai Faraji Nyembo Ommy Dimpoz kumuua kwa maneno msanii Cyrill, sasa yamemrudi baada ya Cyrill naye kuongea yasiyofaa kumhusu Ommy Dimpoz.

Ommy Dimpoz alinukuliwa katika kituo kimoja cha redio akisema kuwa Cyrill ni msanii ambaye hafanyi shoo kabisa.

"Huyu jamaa amekosea kwa kwa kukimbilia katika vyombo vya habari na kuzungumza tu, siku nyingine ajipange kabla ya kufanya mahojiano yoyote, kwani ukiwa msanii wewe ni kioo cha jamii, haifai kuongea kila linalokuja kichwani mwako" alisema Cyrill
Bifu hili jipya kati ya wasanii hawa limetokana na kuzuiwa kwa Cyrill kufanya show na BASATA siku ya Jumapili iliyopita pale Club Maisha akidaiwa hana kibali kwani ni raia wa Kenya.
Ommy Dimpoz naye alikuwa na shoo yake siku hiyo Billcanas.
Baadaye Ommy Dimpoz alifunguka kwenye vyombo vya habari na kusema Cyrill anatangaza kuwa yeye ndiye kamfanyia fitna ili asifanye shoo hiyo, jambo alilokanusha.

Sunday, May 27, 2012

MHESHIMIWA VICK KAMATA ATOA MSAADA WA BAISKELI KWA WALEMAVU MKOA WA GEITA WILAYA YA NYAKAMWAGA

Mbunge wa viti maalum CCM mkoani Geita, Mh Vick Kamata akisalimiana na mtoto ambaye ana ulemavu wa mguu kwa muda wa miaka 15 tangu sasa tangu alipozaliwa huyu ni mmoja kati ya waliokabidhiwa baiskeli ili kuwawezesha katika harakati za maisha hususani kwa kijana huyu kwenye kuisaka elimu.
Victoria Foundation kwa muda mrefu sasa imekuwa ikifanya jitihada kuyawezesha makundi mbalimbali katika jamii ambapo mpaka sasa wananchi wengi katika makundi hayo yameweza kukuza vipato vyao.
Kundi hili katika jamii limeweza kupata baiskeli ambazo ni imani kwamba zitafanikisha kurahisisha harakati mbalimbali za kujikwamua kiuchumi na kushiriki ujenzi wa taifa letu la Tanzania kwani walemavu wakiwezeshwa naaam wanaweza.
 Baiskeli 30 zilizotolewa na Victoria Foundation kwa wananchi wenye ulemavu wilayani Nyakamwaga mkoa mpya wa Geita.
Ni baadhi ya walemavu wakiwa wamepanda baiskeli zao baada ya kukabidhiwa.
Ni kama fikra za ndugu zetu hawa zinasema "Sasa tutashiriki vyema kwenye shughuli mbalimbali za jamii yetu"

Ni wazi kuwa kijana huyu alikuwa akipata taabu sana kwenda shule hasa ukizingatia shule nyingi vijijini ziko mbali na makazi ya watu kwa mpango huu wa uwezeshaji kutoka Victoria Foundation utamsaidia kuepukana na adha hizo. 
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...